Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Anapotusamehe, je, Anasahau?

Mungu Anapotusamehe, je, Anasahau?

Umukaribie Mungu

Mungu Anapotusamehe, je, Anasahau?

KWA kifupi, jibu ni ndiyo. Yehova anaahidi hivi juu ya watu ambao anakubali: ‘Nitalisamehe kosa lao, na zambi yao sitaikumbuka tena.’ (Yeremia 31:34) Kwa kusema hivyo, Yehova anatuhakikishia kama anaposamehe wafanya zambi wanaotubu, yeye hakumbuke tena zambi zao. Lakini, je, hilo linamaanisha kama Muumbaji wa ulimwengu wote hana uwezo wa kukumbuka zambi alizosamehe? Maneno ya nabii Ezekieli yanatusaidia kuelewa namna Mungu anavyosamehe na kusahau.​—Soma Ezekieli 18:19-22.

Yehova alitumia nabii Ezekieli ili kutangaza hukumu juu ya wakaaji wa Yuda na Yerusalemu ambao hawakuwa waaminifu. Taifa nzima liliacha kumuabudu Yehova na matendo ya jeuri yalienea katika muji. Yehova alitabiri kama Wababiloni wataharibu Yerusalemu. Lakini alipokuwa akitangaza hukumu hiyo, alitoa pia tumaini. Kila mutu alipaswa kuchagua; kila mutu angehukumiwa kwa sababu ya matendo yake.​—Mustari wa 19, 20.

Basi, ingekuwa namna gani ikiwa mutu aliacha mabaya na kutenda mema? Yehova alisema hivi: ‘Kwa habari ya muovu, ikiwa atageuka na kuziacha zambi zake zote ambazo ametenda naye hakika ashike sheria zangu zote na kutenda haki na uadilifu, hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.’ (Mustari wa 21) Kwa kweli, Yehova alikuwa “tayari kusamehe” mutenda zambi aliyetubu kwelikweli na kuacha njia yake mbaya.​—Zaburi 86:5.

Tuseme nini juu ya zambi zake alizotenda? Yehova alisema hivi: “Makosa yake yote ambayo ametenda​—hayo hayatakumbukwa juu yake.” (Mustari wa 22) Ona kama zambi za mutu aliyetubu ‘hazingekumbukwa.’ Hilo linamaanisha nini?

Katika Biblia, neno la Kiebrania linalotafsiriwa “kukumbuka” linaweza kumaanisha mambo mengi, si kukumbuka tu mambo ya zamani. Juu ya neno hilo, kitabu kimoja kinasema hivi: “Kwa kweli, mara nyingi, neno hilo linatoa wazo la kitendo ao mutu anayechukua hatua ili kutenda.” Kwa hiyo, “kukumbuka” kunaweza kumaanisha “kutenda.” Wakati Yehova anasema kama zambi za mutenda zambi aliyetubu ‘hazitakumbukwa,’ anapenda kusema kama hatachukua hatua juu ya mutu kwa sababu ya zambi zake; hatamulaumu ao kumuazibu mutu huyo kwa sababu ya zambi hizo ambazo amekwisha kutubu. *

Maneno ya Ezekieli 18:21, 22 yanatugusa moyo sana kwa sababu yanaeleza kadiri Mungu anavyosamehe. Yehova anaposamehe zambi zetu, hawezi tena kutuona kuwa wenye zambi wakati ujao. Lakini, zambi za watu waliotubu anazitupa nyuma ya mugongo wake. (Isaya 38:17) Ni kama vile anafuta ao kuondoa kabisa zambi hizo.​—Matendo 3:19.

Kwa sababu sisi ni wanadamu wasio wakamilifu, tunafanya zambi mara nyingi, kwa hiyo, tunahitaji kabisa rehema ya Mungu. (Waroma 3:23) Yehova anataka tujue kama iko tayari kutusamehe, ikiwa tunatubu kwelikweli. Na anapotusamehe, anasahau​—ni kusema kama, haendelee kukumbuka​-kumbuka zambi zetu ili kutulaumu ao kutuazibu tena. Hilo ni wazo lenye kutia moyo sana! Rehema ya Mungu inakusukuma umukaribie zaidi, sivyo?

Tafazali, mwezi huu wa 7, soma Maandiko haya katika Biblia:

Ezekieli sura ya 6 mupaka sura ya 20

[Maelezo ya chini]

^ Vilevile, “kukumbuka zambi” kunaweza kumaanisha “kuchukua hatua juu ya watenda zambi.”​—Yeremia 14:10.