Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Viumbe wa Kiroho: Ni Marafiki ao Maadui Wetu?

Viumbe wa Kiroho: Ni Marafiki ao Maadui Wetu?

Neno la Mungu Linafundisha Nini?

Viumbe wa Kiroho: Ni Marafiki ao Maadui Wetu?

Habari hii inazungumuzia maulizo fulani ambayo labda umejiuliza na inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu katika Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia upate majibu ya maulizo hayo.

1. Malaika ni nani?

Malaika ni viumbe wa kiroho wanaoishi mbinguni. Uzima wao haufanane hata kidogo na uzima wa wanadamu. Mungu wa kweli, ambaye ni roho pia, aliwaumba malaika mbele ya kuumba dunia. (Ayubu 38:4, 7; Mathayo 18:10) Yehova anazungukwa na malaika waaminifu wengi sana.​—Soma Zaburi 103:20, 21; Danieli 7:9, 10.

2. Je, malaika wanasaidia watu?

Malaika walimusaidia mwanaume mwenye haki anayeitwa Loti. Mwanaume huyo aliishi katika muji ambao Mungu alikusudia kuharibu kwa sababu ya mambo mabaya ambayo watu wa muji huo walikuwa wakifanya. Malaika wawili walimuonya Loti na jamaa yake wakimbie muji huo. Watu fulani waliona jambo hilo kuwa muzaha na wakalizarau. Lakini, Loti na binti zake walipona kwa sababu walitii onyo ambalo Mungu aliwatolea kupitia malaika.​—Soma Mwanzo 19:1, 13-17, 26.

Biblia inasema kama leo malaika wanasaidia na kuongoza watu waaminifu wanaohubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Kuhubiri habari njema kunamaanisha pia kuwaonya watu. Kama vile onyo ambalo malaika walimutolea Loti, onyo hilo si jambo la muzaha. Ni Mungu ndiye analitoa kupitia malaika.​—Soma Ufunuo 1:1; 14:6, 7.

Mungu anaweza kutumia malaika ili watutie nguvu tunapopambana na majaribu. Alitumia malaika ili amutie Yesu nguvu.​—Soma Luka 22:41-43.

Hivi karibuni Mungu atatumia malaika ili kuharibu watu wabaya wanaoletea wengine mateso. Itakuwa kitulizo kabisa kwa wanadamu.​—Soma 2 Wathesalonike 1:6-8.

3. Mashetani wanachochea watu namna gani?

Kama vile tu watu wengi duniani wamekataa kumutii Mungu kwa kutenda mabaya, vilevile malaika wengi mbinguni wamekataa kumutii Mungu. (2 Petro 2:4) Malaika hao ambao wamekataa kumutii Mungu wanaitwa mashetani. Kapita wao ni Shetani Ibilisi. Shetani na mashetani wake wanawapoteza wanadamu.​—Soma Ufunuo 12:9.

Shetani anatumia biashara zenye kujaa mambo maovu, serikali ao guvernema za wanadamu, na dini za uongo ili kuwachochea watu wasimutii Mungu. Kwa hiyo, ikiwa leo kuna ukosefu wa haki, jeuri na mateso, ni Shetani ndiye anayechochea mambo hayo.​—Soma 1 Yohana 5:19.

4. Mashetani wanadanganya watu namna gani?

Shetani anadanganya watu wengi kupitia mafundisho yanayosema kama watu wanapokufa wanakuwa roho wanaoweza kuzungumuza nao. Lakini, Biblia inasema kama watu waliokufa hawawezi kufanya jambo lolote. (Mhubiri 9:5) Mara nyingi mashetani wanadanganya watu kwa kuiga sauti ya watu waliopenda ambao wamekufa. (Isaya 8:19) Mashetani wanadanganya watu wengine kwa kutumia watu wanaozungumuza na pepo, waaguzi, wale wanaotabiri mambo, na wale wanaochunguza nyota. Neno la Mungu linatuonya tuepuke mazoea hayo. Tunapaswa kutupa kitu chochote kinachoweza kutufanya tuwe na uhusiano na mashetani ao mambo ya uchawi.​—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10, 11; Matendo 19:19.

Ikiwa tunamupenda Yehova, hatutawaogopa mashetani. Tunapojifunza Neno la Mungu na kufanya kama linavyosema, tunamupinga Ibilisi na tunamukaribia Mungu. Yehova ana nguvu zaidi kuliko mashetani. Malaika wake waaminifu wanaweza kututia nguvu tunapozihitaji.​—Soma Zaburi 34:7; Yakobo 4:7, 8.

Ili kupata habari zingine, usome sura ya 10 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.