Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | KUNA MUTU ANAYEWEZA KUJUA WAKATI UNAOKUJA?

Matabiri Fulani Yametimia, Mengine Mengi Hayakutimia

Matabiri Fulani Yametimia, Mengine Mengi Hayakutimia

Ungependa kujua wakati wako unaokuja? Wazo la kutafuta kujua wakati unaokuja linavutia watu wengi. Kuna watu wengi wanaotabiri matukio ya wakati unaokuja, na wanapata matokeo mbalimbali. Chunguza mambo yanayofuata:

  • WANASAYANSI wanatumia vifaa vya hali ya juu na feza nyingi sana ili kutabiri mambo mbalimbali, kwa mufano matokeo ya kuchafuka kwa hewa juu ya dunia na ikiwa mvua itanyesha kesho katika eneo lenu.

  • WACHUNGUZI WA HALI YA JUU wanatabiri mabadiliko katika biashara na siasa. Warren Buffett, mumoja kati ya matajiri sana wa duniani, aliweza kutabiri bila kukosea mabadiliko katika biashara na hivyo watu fulani walimuita nabii. Nate Silver, muchunguzi mwengine, alifasiria hesabu fulani zilizomusaidia kutabiri juu ya kila kitu kuanzia siasa za inchi ya Amerika mupaka zawadi za sinema za Hollywood.

  • MAANDISHI YA ZAMANI yameelezwa kuwa unabii. Watu fulani wanaona kuwa maandishi yasiyo wazi ya Michel de Notredame (Nostradamus) ya kati ya mwaka wa 1501 na 1600 yanatimizwa leo. Kalenda ya Wamaya iliisha tarehe 21 Mwezi wa 12, 2012; watu fulani walieleza kwamba tarehe hiyo kutakuwa matukio ya uharibifu mukubwa duniani.

  • VIONGOZI WA DINI wakati fulani wanatabiri kwamba kutakuwa matukio mabaya sana duniani pote ili kuonya watu na kupata wafuasi. Harold Camping, nabii aliyetabiri maangamizi tu pamoja na wafuasi wake walitangaza sana kwamba dunia ingeharibiwa katika mwaka wa 2011. Lakini dunia ingali mupaka leo.

  • WACHAWI FULANI wanasema kwamba wana uwezo wa pekee wa kutabiri mambo ya wakati unaokuja. Edgar Cayce na Jeane Dixon wote wawili walitabiri bila kukosea mambo fulani juu ya matukio kati ya mwaka wa 1901 na 2000. Kila mumoja wao alitabiri pia mambo mengi yenye hayakutimia. Kwa mufano, Dixon alitabiri kwamba Vita ya Tatu ya Ulimwengu ingetokea katika mwaka wa 1958, na Cayce alitabiri kwamba muji wa New York ungezama ndani ya bahari katika mwaka wa 1975 hivi.

Kuna njia yoyote yenye kutegemeka ya kujua wakati unaokuja? Ulizo hilo ni lenye kufaa. Ikiwa ungekuwa na uwezo wa kuona mbele ya wakati matukio ya wakati unaokuja, maisha yako yangekuwa tofauti.