Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Koreshi Mkuu

Koreshi Mkuu

Kulingana na kalenda ya kisasa, usiku wa Oktoba 5/6, 539 K.W.K., jambo lililoonekana kuwa haliwezekani lilitendeka katika jiji la Babiloni, mji mkuu wa Milki ya Babiloni. Katika usiku huo wenye matukio muhimu, jiji hilo lilipinduliwa na jeshi la Wamedi na Waajemi, likiongozwa na Mfalme Koreshi Mwajemi, ambaye pia anaitwa Koreshi Mkuu. Mbinu aliyotumia ilikuwa ya werevu sana.

JINSI KORESHI ALIVYOTEKA BABILONI

“Koreshi alipoamua kulishambulia Babiloni, tayari lilikuwa jiji lililotukuka zaidi kati ya majiji ya Mashariki ya Kati—labda hata kati ya majiji yote ulimwenguni,” kinasema kitabu Ancient World Leaders—Cyrus the Great. Mto Efrati ulipitia Babiloni na pia maji ya mto huo yalijaa kwenye mahandaki yaliyozunguka kuta kubwa za jiji hilo—na hilo lilifanyiza mfumo wa ulinzi uliofanya jiji hilo lionekane kuwa haliwezi kushindwa.

Wanaume wa Koreshi walibadili mkondo wa mto huo umbali fulani kabla ya kufika Babiloni na hivyo kufanya kiwango cha maji katika jiji hilo kupungua. Kisha wanajeshi wakapita ndani ya mto huo na kufika kwenye malango ya jiji, yaliyokuwa yameachwa wazi, na kuliteka Babiloni bila upinzani mkubwa. Kulingana na wanahistoria Wagiriki Herodoto na Xenophon, usiku walioshambuliwa, Wababiloni walijihisi wakiwa salama nyuma ya mfumo wa ulinzi wa jiji lao, na hata wengi wao walikuwa katika karamu, kutia ndani mfalme! (Ona sanduku lenye kichwa  “Maandishi ya Mkono Yako Ukutani.”) Isitoshe, mashambulizi ya Koreshi yalitimiza unabii wa Biblia wenye kushangaza.

Biblia ilitabiri ushindi wa Koreshi dhidi ya Babiloni

 UNABII WENYE KUSHANGAZA

Unabii huu mbalimbali wa Isaya ni wenye kushangaza sana kwa kuwa uliandikwa miaka 200 hivi kabla ya wakati ulipotimia—huenda miaka 150 hivi kabla ya Koreshi kuzaliwa! Fikiria yafuatayo:

KUKOMBOLEWA KIMUUJIZA

Mapema, katika mwaka wa 607 K.W.K., majeshi ya Babiloni yaliteketeza jiji la Yerusalemu na kuwapeleka waokokaji wengi uhamishoni. Wayahudi wangekuwa mateka kwa muda mrefu kadiri gani? Mungu alisema hivi: “Miaka 70 itakapotimia nitatoza hesabu juu ya mfalme wa Babiloni na juu ya taifa lake . . . nami nitaifanya kuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.”—Yeremia 25:12.

Kama ilivyotajwa, Koreshi aliliteka Babiloni mnamo 539 K.W.K. Muda mfupi baada ya hapo, aliwaachilia Wayahudi, na baadhi yao waliwasili nyumbani kwao mnamo 537 K.W.K.—miaka 70 kamili baada ya uhamisho wao. (Ezra 1:1-4) Mwishowe, Babiloni likawa “mahame yenye ukiwa”—na hivyo kuthibitisha tena usahihi wa unabii wa Biblia.

KWA NINI HABARI HII IKUPENDEZE?

Fikiria hili: Biblia ilitabiri (1) Wayahudi wangepelekwa uhamishoni kwa miaka 70, (2) ushindi wa Koreshi dhidi ya Babiloni na mbinu muhimu ambazo angetumia, na (3) ukiwa wa Babiloni ambao ungetukia baadaye. Ujuzi kama huo wa mapema haungeweza kutoka kwa wanadamu! Mkataa unaopatana na akili zaidi ni huu: “Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu.” (2 Petro 1:21) Kwa kweli, tunapaswa kuichunguza Biblia.

^ fu. 36 Maneno hayo yanarejelea kipimo cha uzito wa pesa. Kwa maelezo zaidi, ona sura ya 7 ya kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.