Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Ndoa inawezaje kuwa na furaha?

Ushauri wa Biblia kuhusu ndoa ni wenye kutegemeka kwa sababu unatoka kwa Mwanzilishi wa ndoa, Yehova Mungu. Inatufundisha jinsi ya kuwa na sifa zinazoweza kufanya ndoa iwe yenye furaha na inatuonya kuhusu mitazamo inayoweza kuharibu ndoa. Pia, inatufundisha jinsi ya kuwasiliana ili tuzidishe furaha katika ndoa.Soma Wakolosai 3:8-10, 12-14.

Mume na mke wanapaswa kuheshimiana. Kila mmoja akitimiza wajibu aliopewa na Mungu, ndoa yao inaweza kuwa na furaha.Soma Wakolosai 3:18, 19.

Ni nini kinachofanya ndoa idumu?

Wenzi wa ndoa wanaweza kuishi pamoja ikiwa wanapendana. Mungu anatufundisha jinsi ya kupendana. Yeye na Mwanaye Yesu wameweka mfano bora wa upendo wa kujidhabihu.Soma 1 Yohana 4:7, 8, 19.

Mume na mke watafurahia kuishi pamoja ikiwa wataheshimu mpango wa ndoa ulioanzishwa na Mungu. Mungu alianzisha ndoa iwe muungano wa kudumu kati ya mume na mke ili kulinda familia. Ndoa inaweza kudumu kwa sababu Mungu aliumba mume na mke wakamilishane kimwili na kihisia. Pia, aliwaumba kwa mfano wake, wakiwa na uwezo wa kuiga upendo wake.Soma Mwanzo 1:27; 2:18, 24.