Ona video zinazopatikana

Naweza Kufanya Nini juu Nikuwe Shahidi wa Yehova?

Naweza Kufanya Nini juu Nikuwe Shahidi wa Yehova?

 Yesu alionyesha mambo yenye mutu anaweza kufanya juu afikie kuwa Shahidi wa Yehova na ile mambo inapatikana pia mu Matayo 28:19, 20. Ile andiko inaonyesha mambo yenye mutu anaweza kufanya juu akuwe mwanafunzi wa Yesu. Kuwa mwanafunzi wa Yesu kunatia ndani kusema ao kutoa ushahidi juu ya Yehova.

 Jambo ya 1: Ujifunze mambo yenye Biblia inafundisha. Yesu aliamuru wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi . . . , na kuwafundisha.’ (Matayo 28:19, 20) Neno yenye kutafsiriwa “mwanafunzi” inamaanisha moja kwa moja “mwenye kujifunza.” Biblia, na zaidi sana mafundisho ya Yesu Kristo yenye kuwa ndani, iko na habari zenye uko nazo lazima juu ukuwe na maisha ya furaha na yenye maana. (2 Timoteo 3:16, 17) Tuko na furaha ya kukusaidia ujifunze mambo yenye Biblia inafundisha kupitia programu yetu ya kujifunza Biblia na watu, bila kulipa.​—Matayo 10:7, 8; 1 Watesalonike 2:13.

 Jambo ya 2: Utumikishe mambo yenye uko unajifunza. Yesu alisema kama wale wenye kujifunza wanapaswa ‘kushika mambo yote yenye aliamuru.’ (Matayo 28:20) Ni kusema, funzo yako ya Biblia haipaswe kukusaidia tu ukuwe ujuzi, lakini inapaswa pia kukusaidia ufanye mabadiliko ya mukubwa sana mu mawazo na matendo yako. (Matendo 10:42; Waefeso 4:22-​29; Waebrania 10:24, 25) Kwa hiyo, wale wenye wanashika amri za Yesu wanafikia kuamua sasa wao wenye kumufuata na kutoa maisha yao kwa Yehova Mungu.​—Matayo 16:24.

 Jambo ya 3: Ubatizwe. (Matayo 28:19) Mu Biblia, ubatizo unalinganishwa na kuzikwa. (Linganisha na Waroma 6:2-4.) Ile ni alama yenye kuonyesha kama mutu amekufa, ni kusema, ameacha maisha yake ya zamani na anaanza sasa maisha ya mupya. Kwa hiyo, ubatizo wako ni tangazo ya mbele ya watu wote yenye kuonyesha kama umetiza mambo mbili ya kwanza yenye Yesu alionyesha na kama unaomba Mungu akupatie zamiri safi.​—Waebrania 9:14; 1 Petro 3:21.

Nini njo itanisaidia kujua kama niko tayari kwa ajili ya kupata ubatizo?

 Ongea na wazee wa kutaniko. Watazungumuza na weye ili kujua kama unaelewa kabisa mambo yenye inaombwa ili upate ubatizo, kama uko unatumikisha mambo yenye umejifunza, na kama umejitoa kwa Mungu kwa kupenda, bila kusukumwa na mutu fulani.​—Matendo 20:28; 1 Petro 5:1-3.

Hii mambo tatu inahusu pia watoto wa Mashahidi wa Yehova?

 Ndiyo. Tunakomalisha watoto wetu “katika nizamu na maonyo ya Yehova,” kama vile Biblia inaamuru. (Waefeso 6:4) Lakini, kadiri wako wanakomala, wanapaswa kukamata maamuzi wao wenyewe kuhusu kujifunza, kukubali, na kutumikisha mambo yenye Biblia inafundisha mbele wabatizwe. (Waroma 12:2) Kusema kweli, kila mutu anapaswa kukamata uamuzi wake mwenyewe kuhusu mambo ya ibada.​—Waroma 14:12; Wagalatia 6:5.