Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?

Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?

Je, Kuna Yeyote Anayesikiliza Sala?

“Nilikuwa na shaka kuhusu kuwapo kwa Mungu. Hata hivyo, nyakati nyingine nilijaribu kusali. Sikuwa na hakika ikiwa kuna yeyote aliyenisikiliza, lakini kusema kweli niliamini kulikuwa na mtu anayesikiliza sala. Sikuwa na furaha wala kusudi maishani. Niliogopa kuamini kwamba kuna Mungu kwa sababu nilifikiri ni watu dhaifu tu ndio walioamini Mungu.”​—⁠PATRICIA, * IRELAND.

JE, UMEWAHI kuhisi kama alivyohisi Patricia? Je wewe husali hata kama unatilia shaka kwamba kuna Mungu? Ikiwa ndivyo, basi si wewe peke yako mwenye hisia kama hizo. Fikiria mambo yafuatayo.

▪ Utafiti uliohusisha raia 2,200 wa Uingereza ulionyesha kuwa ni asilimia 22 tu kati ya watu hao wanaoamini kwamba kuna Mungu aliyeumba ulimwengu na ambaye husikiliza sala. Hata hivyo, kati ya watu waliohojiwa, asilimia 55 husali mara chache tu.

▪ Utafiti mwingine uliohusisha watu 10,000 katika nchi mbalimbali ulionyesha kwamba wale wanaodai hakuna Mungu, karibu asilimia 30 kati yao husali.

Kwa Nini Watu Wengi Wana Shaka?

Allan mwanamume kutoka Uingereza anasema hivi: “Nilizoea kusema kwamba siamini kuna Mungu kwa sababu nilifikiri dini huanzishwa kwa kusudi la kuwadhibiti watu au kupata pesa. Vilevile, nilifikiri ikiwa kuna Mungu hakungekuwa na ukosefu mwingi sana wa haki. Hata hivyo, nyakati nyingine ningeketi peke yangu na kusali kwa ‘mtu’ asiyejulikana. Pia, ningejiuliza, ‘Chanzo cha uhai ni nini? ’ ”

Kila mtu mwenye hisia kama hizo ana sababu zake zinazomfanya atilie shaka kama sala hujibiwa. Mara nyingi, wanakuwa na shaka kwa sababu ya kukosa majibu ya maswali kama vile:

▪ Je, kuna Muumba?

▪ Kwa nini mara nyingi dini inachochea watu wafanye mambo mabaya?

▪ Kwa nini Mungu ameruhusu kuteseka?

Ikiwa ungepata majibu ya maswali hayo, je, ungesali ukiwa na uhakika?

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 2 Baadhi ya majina katika mfululizo huu yamebadilishwa.